Translate in your language

Wednesday, March 10, 2010

Multichoice yazindua huduma za Dstv mashuleni

KAMPUNI ya Multchoice  Tanzania, Multchoice  Afrika kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na  Mafunzo ya Ufundi,  imezindua rasmi huduma zake za Dstv  zitakazo kuwa zikitumika kutolea mafunzo kwa wanafunzi.
 
Katika alfa ya uzinduzi huo ulifanyika jana  jijini Dar es Salaam , shule ya Sekondari ya Wasichana ya Jangwani, ilipata fursa ya kipekee kwa kufungua rasmi huduma hiyo.
 
Katika uzinduzi huo uliodhuriwa  ulioudhuriwa na Naibu Katibu Mkuuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ASelestine Gasimbe aliipongeza Multcoice Tanzania kwa kufanikisha msaada huo ambao utakuwa ni chachu ya maendeleo kwa elimu nchini “Nina hakika kwa msaada huu, wanafunzi watapata kujifunza mambo mbalimbali, na kujenga uwezo mkubwa wa kimaendeleo” alisema  Gasimbe.
 
Naye Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Peter Fauel alisema kuwa kwa kufunga kifaa hicho wanafunzi hao watapata fursa za kujifunza mengi  na kufurahia  faida mbalimbali kutoka katika chaneli za kifaa hicho. “Kupitia Dstv, hakika mtapata kuona  vipindi mbalimbali vya ulimwengu mzima na kuweza kujifunza zaidi kupitia humo” alisema Fauel.
 
Multichoice  Tanzania  mbali na shule hiyo ya Sekondari Jangwani, tayari imeweza kufunga na kutoa vifaa mbalimbali katika shule 20 za Tanzania , vifaa hivyo ni pamoja na Satellite ya kisasa, kimang’uzi cha Dstv na televiasheni.
 
Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa Kampuni hiyo, Barbara  Kambogi, alisema kuwa vifaa hivyo ambavyo vimeunganishwa vipindi mbalimbali, vikiwemo vile vya Wanyama, Siasa,Elimu,Taarifa za Habari za makampuni makubwa ya Ulimwengu ikiwemo BBC na vipindi vingine vya maarifa.
 
Chaneli muhimu watakazo faidika nazo wanafunzi hao na kujifunza mambo mbalimbali ni pamoja na ‘Discovery Cahannel, National Geographic,BBC Word, History Channel na Animal Planet alisema Kambogi.
 
Mwisho
 

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)