Translate in your language

Sunday, March 21, 2010

MSAADA!!

MOVENPICK YAIPIGA JEKI HABITAT KWA MAKAZI

 

Na Mwanablog wetu Dar

 

HOTELI ya Movenpick ya jijini Dar es Salaam, imetoa Dolla za Kimarekani 14,000 kwa shirika lisilo la kiserikali la Makazi la Habitat, kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa makazi.

 

Pesa hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki, ikiwa ni kuikubali shirika hilo katika harakati zake za kusaidia wananchi wasio na uwezo wa kujenga nyumba bora kwa ajili ya makazi.

 

Akikabidhi kwa Mkurugenzi wa Habitat nchini, Scott Metzel, mwakilishi wa hoteli hiyo,  Gehan Moustafa, alisema Movenpick bado itaendelea kutoa mchango kwa Habitat kutokana na kazi kubwa inayofanya shirika hilo, kwa ajili ya kusaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kujenga nyumba bora.

 

"Hoteli hii imeweka kipaumbele katika kuisaidia jamii yenye uhitaji hasa katika suala zima la kuwajengea makazi wananchi wasiokuwa na uwezo wa kujanga nyumba bora za kuishi, hivyo Habitat tutaendelea kuwaunga mkonp kwa kazi yao ya kuwajengea nyumba wananchi hao" alisema.

 

Gehan alisema, Hoteli hiyo imekuwa ikifanya kazi na Habitat katika kuwasaidia wananchi, ambapo Agosti 22 mwaka juzi, wameshajenga nyumba  maeneo ya Chamazi, Mbagala.

 

Ambapo malengo ya mwaka huu ni kuongeza nyumba zaidi kwa wakazi wasiokuwa na uwezo lakini pia wanampango wa kupanya wigo sehemu nyingine Afrika.

 

Akipokea msaada huo, Mkurugenzi huyo wa Habitat, Metzel alisema shirika hilo sio la kiserikali ambapo lengo la kuanzishwa ni kuwasaidia wananchi wenye uwezo mdogo wa kujenga nyumba bora kwa ajili ya makazi.

 

Aidha shirika hilo hutoa misaada mbalimbali ikiwa ni pamoja na vifaa vya ujenzi kama vile, Mabati, matofali ilikusaidia ujezi wa nyumba hizo.

 

Alisema kwamba, hadi sasa limeshajenga nyumba bora 250 jijini Dar es Salaam kwa muda wa miezi tisa, lakini pia shirika hilo linatoa mikopo kwa midogomidogo kwa wananchi wenye kipato cha chini kwa ajili ya kujenga nyumba.

 


No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)