Translate in your language

Friday, July 11, 2014

FIFA YATUPILIA MBALI RUFAA YA SUARE

Fifa imetupilia mbali rufaa ya mshambuliaji wa Uruguay na Liverpool Luis Suarez, ya kupinga adhabu ya miezi minne ya kutokujihusisha na shughuli zozote za kandanda, kwa kosa la kumng'ata Giorgio Chiellini wa Italy.
Suarez pia alifungiwa mechi tisa za kimataifa. 
Shirikisho la soka la Uruguay lilielezea adhabu ya Fifa kuwa ni "uamuzi uliopita kiasi" na hakukuwa na "ushahidi wa kutosha".
Suarez sasa anaweza kukata rufaa katika mahakama ya usuluhishi wa michezo.
Fifa pia ilimtoza Suarez faini ya Faranga za Uswisi 100,000.
Suarez aliomba radhi kwa alichokifanya.
Liverpool imekuwa ikishughulikia uhamisho wa mchezaji huyo kwenda Barcelona.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)