Nairobi Mji Mkuu wa Kenya |
Patrick Richer mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya matangazo ya kibiashara ya Sydney maisha yake ni yale wanaoishi wataalamu wa kigeni,akiishi kwenye viunga vya Nairobi vya watu wa kipato cha juu wakizingukwa na kuta refu za ulinzi na kuwekwa kwa usalama wa saa 24.
Lakini hapo mwezi wa Novemba masahibu ya mwishoni mwa juma yakamkuta: genge la wanaume 10 walijipenyeza kwa kuvunja uzio wa nyuma ya nyumba,wakawafunga kamba walinzi wake na kuvamia nyumba yake alfajiri kwa kutaraji kujinyakulia kitita cha fedha taslimu,vito vya tahamani na vitu vyengine vya matumizi.Richer mwenye umri wa miaka 39 alipigwa risasi mara mbili na alifikishwa hospitali na mke wake.Alitangazwa kuwa amekufa mara tu baada ya kufikishwa hospitalini.Majambazi walioivamia nyumba yake walikuwa wamevalia sare za polisi na kwa mujibu wa repoti waliiba televisheni,komyuta za mkononi na simu.
Tukio hilo la kufadhaisha limekuja wakati kukiwa na mwendendo unaozidi kuwa mbaya katika mji mkuu wa Kenya Nairobi ambalo ni wimbi la uhalifu wa kabla ya kipindi cha Krismasi unaotekelezwa na wezi ambao kila kukicha wanazidi kuwa tayari kuuwa kukidhi haja zao.
No comments :
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa