Translate in your language

Wednesday, November 27, 2013

Mbunge anayelelewa na wake zake mama ntilie

Aliyekuwa Mbunge wa Songea mjini kuanzia Oktoba 1985 hadi Aprili 1988 alipofungwa jela miaka 11, Abdulrabi Ali Yusuph (66), amesema tangu atoke gerezani hadi sasa anaomba aonane na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi ama Rais Benjamin Mkapa na hata Rais Jakaya Kikwete lakini hajafanikiwa hadi leo.
Amesema aliomba nafasi ya kumwona Rais Mwinyi akiwa madarakani ili amweleze ya moyoni, lakini hakufanikiwa na aliendelea kuomba amwone Rais Mkapa hakufanikiwa na sasa anaomba amwone Rais Kikwete bado hajajaaliwa.
Alisema hayo katika mahojiano maalumu yaliyofanyika nyumbani kwake Mtaa wa Mfaranyaki mjini Songea ambako anaishi akiwa kwenye nyumba chakavu ya urithi na wake zake wawili pamoja na watoto kadhaa.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)