Translate in your language

Wednesday, April 21, 2010


Picha zaonesha 'wizi' wa kura
Sudan


Wanaharakati wa upinzani nchini Sudan wamesema,
picha ya video iliyosambazwa kwenye tovuti
inathibitisha madai yao ya udanganyifu katika 
uchaguzi.

Wanaharakati hao wanasema video hiyo inaonesha
maafisa wa uchaguzi wakitumbukiza karatasi ndani
ya maboksi ya kupigia kura.

Picha hiyo, ambayo hata hivyo haijathibitishwa rasmi, imewekwa kwenye tovuti na inasambazwa na kundi 
mpja la wanaharakati.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema picha
hiyo si ya kweli na haitafanya uchunguzi wowote 
juu yake.

Uchaguzi huo ulifanywa kufuatia makubaliano ya
amani ya kumaliza mapigano ya wenyewe kwa 
wenyewe yaliyodumu kwa zaidi ya miaka 20.

Matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutolewa 
wiki hii.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)