Translate in your language

Wednesday, April 21, 2010


Uwanja wa Heathrow wafunguliwa


Ndege hatimaye zimeanza kutua na kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Heathrow mjini
London, ambao ndio uwanja wenye shughuli nyingi zaidi barani ulaya, baada ya uingereza
kuondoa vikwazo dhidi ya usafiri wa ndege.

Marufuku hiyo imekuwepo tangu mlipuko wa volcano nchini Iceland wiki moja iliopita.
Nchi kadhaa pia zimelegeza vikwazo vya usafiri wa ndege lakini katika mataifa mengine 
marufuku hiyo bado inaendelea kudumishwa.

Nusu ya idadi ya safari za ndege zilirejelewa jana na maelfu ya abiria bado wamekwama 
katika viwanja kadhaa vya ndege duniani.

Mlipuko huo wa Volcano nchini Iceland unaendelea lakini viwango vya mawingu ya majivu 
vimepungua.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)