Translate in your language

Saturday, March 20, 2010

TRAWU,NAO WATANGAZA MGOMO KUUNGANA NA TUCTA

Breakin News!!

 

TRAWU,NAO WATANGAZA MGOMO KUUNGANA NA TUCTA

 

 

Na  Mwanablog wetu Dar

 

 

CHAMA cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) imetoa tamko rasmi ya kuunga mkono mgomo uliotangazwa na Chama cha Wafanyakaazi Nchini (TUCTA) wa kugoma nchi nzima.

 

Akizungumza na waandishi wa Habari jana, jijini Dar es Salaam, katika ofisi za makao makuu ya TUCTA, Katibu mkuu wa Trawu, Sylvester Rwegasira alisema kuwa wameamua kuungana na TUCTA  kushiriki mgomo huo.

 

Rwegasira alisema kuwa,  wao kama wanachama halali wa TUCTA, wameamua kuungana na vyama vilivyo katika umoja huo, vilivyotangaza kuungana na mgomo huo uliopangwa kufanyika nchi nzima.

 

"Sisi hatujashinikizwa na mtu, bali kwa kuzingatia misingi ya katiba na tukiwa wanachama halali wa TUCTA, tumetangaza rasmi kuwaunga mkono, kwa kuchoshwa na  mifuko ya hifadhi ya jamii, yakiwemo NSSF na PPF." Alisema Rwegasira.

 

Kwa kile alichodai kuwa, mashirika hayo ndiyo chanzo kikuu cha kurudisha nyuma maswala yote ya wafanyakazi nchini, ikiwemo kufanya ufisadi mkubwa wa kuwakata makato makubwa pamoja na unmyonyaji mkubwa katika mishahara yao, huku kima cha mishahara bado tatizao, Rwegasira alisema kuwa uwepo wa mashirika hayo ni kikwazo  cha maendeleo ya wafanyakazi wa chini.

 

"Mashirika ya PPF na NSSF, yanaongoza kwa kukata makato makubwa ya wafanyakazi huku, lakini mfanyakazi anapokuja kustaafu, mafao yake anayolipwa hayaendani na hali halisi ya kutumikia kwake kufuatia mashirika hayo kukata makatio makubwa" alisema.

 

Aliendelea kusema kuwa, mashirika hayo yamekuwa yakikata makato mengi na makubwa wafanyakazi ambao mishahara ambayo  ni midogo, huku wakijinufaisha katika kujenga majengo makubwa yakiwemo vyuo na pamoja na miradi ya majengo, pamoja na kukopesha wabunge fedha za wavuja jasho ambazio wao wanazifanyia kazi za kifisadi" alisema Rwegasira.

 

 


No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)