RAIS mteule wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dk.John Pombe Magufuli,anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani,ambayo kitaifa inatarajiwa kufanyika mkoani hapa desemba mosi mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake jana,mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,alisema maadhimisho hayo yanatarajiwa kuanza novemba 24 mwaka huu kwenye viwanja vya peoples mjini hapa, na yatazinduliwa rasmi novemba 25.
Alisema katika wiki ya maadhimisho hayo,wadau mbalimbali watapata fursa ya kuonyesha shughuli wanazofanya kuhusiana na mapambano dhidi ya UKIMWI,na wananchi pia watapata fursa ya elimu dhidi ya UKIMWI na upimaji wa VVU.
“Ikumbukwe kuwa katika juma la maadhimisho hadi siku ya kilele,tunategemea kuwa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa watakaojumuika nasi katika maadhimisho hayo.Lengo likiwa ni kuona shughuli na huduma mbalimbali zinazohusu masuala ya UKIMWI”,alisema.
Mkuu huyo wa mkoa,alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wakazi wa mkoa huu na wadau wote wa maendeleo,kujitokeza kwa wingi na kushiriki kwa dhati katika kufanikisha maadhimisho na kilele cha siku ya UKIMWI duniani,ambayo kitaifa yataadhimishwa viwanja vya peoples mjini Singida.
Aidha,aliwaomba waandishi wa habari,kuusaidia mkoa kwa kusambaza ujumbe huu zaidi,ili uwafikie wananchi wengi zaidi.Vile vile amesisitiza pia wananchi wa mkoa wa Singida,kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo.
Dk.Kone,alisema;“Singida bila maambukizi mapya ya UKIMWI,Bila vifo vitokanavyo na UKIMWI na bila Unyanyapaa na Ubaguzi,Inawezekana”kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake”.
No comments :
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa