Translate in your language

Thursday, September 11, 2014

UZINDUZI WA COKE STUDIO AFRICA WAFANA DAR


'Coke Studio Africa' msimu wa pili
Vanessa Mdee, Shaa, Joh Makini Diamond 'live' TBC1,TBC2
NA ANDREW CHALE
Mwanamitindo Rio Paul (kulia) akiwa na rafiki zake muda mfupi baada ya uzinduzi wa msimu wa pili wa  Coke studio Africa, Hyatt Hotel, jijini dar es Salaam.
Kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola,  jana usiku ilizindua  msimu wa pili wa onyesho la runinga lijulikanalo kama  'Coke Studio Africa' ambalo linatarajiwa konyeshwa kila Jumatatu na kituo cha Shirika la Utangazaji cha TBC.
Akizungumza na wandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt jijijini Dar es Salaam, Meneja bidhaa wa Coca-Cola Tanzania, Maurice Njowoka alisema, ni furaha na fahari kwa watanzania na waafrika kwa ujumla kwa kukutana pamoja na kuonyesha uwezo wa vipaji vyao hivyo, ambapo watu watapata kuona na kujifunza vipaji na radha nzuri kutoka kwa wasanii 24 wa bara la Afrika.
Wanamuziki  Vanessa Mdee, Jo Makini na Shaa wakiwa katika picha ya pamoja kwenye 'red Carpet  wakati wa uzinduzi huo.
"Muziki ni lugha isiyo na mipaka na njia muhimu ya kuonyesha hisia na furaha, tungependa kusambaza furaha Barani Afrika kupitia muziki kwa kushirikiana na wasanii," alisema Njowoka.
Alisema, ujumbe wa msimu wa mwaka huu ni 'Ushirikiano  wa Afrika, muziki wa afrika', ambapo pia mbali na wasanii nyota pia wameweza kushirikisha bendi, watayarishaji muziki na madj bora wa bara la Afrika.
Njowoka aliwataja wasanii hao kwa mwaka huu na nchi zao kwenye mabano ni pamoja na  Flavor Nabania, Omawumi, Waje, Burna Boy, Chidima, Olamide, Iyanya, Seyi Shay,Yemi Alade na Phyno (wote kutoka Nigeria),  wengine ni Fena Gitu, Rabbit, Victoria Kimani na Jay A (Wote kutoka Kenya),  Navio, Jacie Chandiru na Lilian Mbabazi (Kutoka Uganda),  John Makini, Shaa, Diamond na Vanessa Mdee (Kutoka Tanzania). Wengine ni Neyma, Jose Valdemiro na  Marllen (Msumbiji) huku watayarishaji wa muziki ni Silvastone (Ghana), Chopstix na Afrologic (Nigeria), Kevin Provoke,Kagwe Mugai na Owuor Arunga (Kenya) na wengieo.
Kutoka kushoto ni Joh Makini, Shaa, Bukuku (Mc wa shughuli hiyo), Maurice (bland meneja wa Coca-cola) na Vanessa Mdee.

Hata hivyo, mbali na kuonyeshwa kila Jumatatu kupitia runinga ya TBC,  mashabiki wanaweza kufuatilia pia kupitia tovuti ya Coke studio ambayo ni www.cokestudioafrica.com.
Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na mastaa mbalimbali wakiwemo wanamitindo, wabunifu, mamiss, wasanii wa filamu, muziki, vichekesho.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)