Translate in your language

Friday, January 3, 2014

MASHAMBULINZI MCHINI KENYA

Nchini Kenya watu 10 wamejeruhiwa wakati washambuliaji waliporusha guruneti ndani ya mkahawa mmoja katika mji wa pwani wa Mombasa na kuzusha hofu ya usalama katika eneo hilo tete.

Mkuu wa polisi mjini Diani, Jack Ekakuro, amesema washambuliaji hao waliilenga baa moja iitwayo Tandoor mjini Diani mapema leo, wakati ilipokuwa bado imefurika watu waliokuwa wakiendelea kusherehekea mwaka mpya. Hii ni sehemu ya mlolongo wa mashambulizi, ikiwa ni pamoja na lile la bomu kwenye basi moja katika mtaa wa Eastleigh mjini Nairobi mwezi uliopita, hali inayowatia wasiwasi Wakenya wengi.

chanzo: DW idhaa ya kiswahili 

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)