Translate in your language

Tuesday, January 28, 2014

MAHMOUD THABIT KOMBO KUUNGURUMA LEO BUSTANINI


MAHMOUD THABIT KOMBO KUUNGURUMA LEO UWAMJA WA  BUSTANINI


Na Andrew Chale, Zanzibar

CHAMA cha Mapinduzi CCM, leo Januari 28, kinatarajia kufanya kampeni yake ya Sita (6) ya mkutano wa hadhara kwenye eneo la uwanja wa  Bustanini, katika kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki,  ambapo mgeni rasmi wa kumnadi Mgombea anatarajiwa kuwa, Mwenyekiti wa Mkoa wa Magharibi wa CCM, Mohammed Yusufu Mrefu.

 Akielezea mkutano huo wa Sita wa hadhara, unaotarajiwa kuwa majira ya Saa kumi jioni, eneo hilo la Bustanini, Mahmod Thabit Kombo ,  aliwaomba wananchi wa wa Kiembesamaki kufika kwa wingi kwenye mkutano huo, ambapo pia kutakuwa na shamrashamra mbalimbali zitakazoanza majira ya Saa Nane, mchana. Hivyo amewaomba wananchi  kujitokeza kwa wingi ilikumsikiliza na kuzijua sera za Chama katika kuwaletea maendeleo.

"Leo Januari 28, nawaomba  wananchi wa Kiembesamaki, kujitokeza  kwa wingi eneo la Bustanini.. ilikusikiza sera , Ilani na mipango endelevu tuliyojipangia ndani ya chama" alisema Mahmoud Thabit Kombo.

Aidha, aliwaomba wananchi wa Jimbo hilo,  ifikapo Februari 2, 2014 siku ya Jumapili, kumpa kura za NDIYO, ili awe Mwakilishi wao atakayeenda kuwatetea Bungeni  kwenye Baraza la Wawakilishi, sambamba na kumaliza kero zinazowakabiri.

Baadhi ya mambo, mbalimbali anatarajia kuzungumzia siku ya leo kwenye mkutano huo ikiwemo kero za maji, elimu, kuwezesha vijana, akinamama na jamii nzima ya jimbo hilo la Kiembesamaki, pindi watakapomchagua kuwa mwakilishi wao.

 Mwisho

Picha mgeni rasmi Yusuf Mrefu
 na Picha za Mahmoud Thabit kombo


No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)