Translate in your language

Monday, December 23, 2013

Fw: MAMA MITINDO ASIA IDAROUS KHAMSI: KUFANYA BONGE LA ‘PARTY’ NYUMBANI LOUNGE, DESEMBA 24


MAMA MITINDO ASIA IDAROUS KHAMSI: KUFANYA BONGE  LA 'PARTY' NYUMBANI LOUNGE, DESEMBA 24
HAPPY BIRTHDAY  ASIA IDAROUS KUFANYIKA DESEMBA 24,  NDANI YA NYUMBANI LOUNGE, DAR
 Na Andrew Chale.
DESEMBA 24 'kesho' Jumanne kutakuwa hakutoshi ndani ya mgahawa na ukumbi wa kisasa wa Nyumbani Lounge kwenye bonge la 'Party' ya kuzaliwa kwa Mama Mitindo nchini Tanzania, Asia Idarous Khamsin, atakapokuwa akitimiza miaka 54.
Party hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na  mastaa mbali mbali  wakiwemo wa filamu, muziki, mitindo na wabunifu.
 Akizungumza na mtandao huu, Asia Idarous ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fabak Fashion, na muandaaji wa onyesho kubwa la Kila mwaka la Mavazi lijulikanalo kama … Usiku wa Khanga za Kale, anasema kuwa tayari mandalizi yameshakamilika na wadau mbali mbali wanatarajia kuhudhuria kwenye 'party' hiyo itakayokuwa ya aina yake.
"Kesho Desemba 24, Ni siku yangu ya kuzaliwa, Namshukuru Mungu kwa neema zake kufika hadi leo hii kwa ulinzi na muongozo wake, leo  hii mimi kufikia hapa na kutimiza miaka hii 54" alisema Asia Idarous.
Akitoa nasaha zake kwa wabunifu wa mitindo wanaochipukia hapa nchini, Asia aliwataka wasivunjike moyo kwani kazi hiyo inahitaji uvumilivu na maalifa. "Namshukuru Mungu kwa kufikia hapa leo hii na hakika nitaendeleza fani hii pia nawaomba wabunifu na wanamitindo wanaochipukia kuwa na hali ya ushirikiano, kusaidiana, kuchapa kazi  na kuwa na 'tojo' safi" alisema  Asia Idarous Khamsin.
Aidha, Asia Idarous alisema kuwa milango ipo wazi kwa wabunifu wa mitindo kupata ushahuri wake kwa watakaotaka huku akiwaombea wafike mbali katika kuendeleza gurudumu la mitindo hapa nchini.
Mwisho.



No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)