Translate in your language

Thursday, August 8, 2013

Moto uwanja wa ndege wa Kenya wadhibitiwa

Moto mkubwa katika uwanja mkuu wa ndege jijini Nairobi ambao umeharibu eneo muhimu la kurukia na kutulia ndege na kuilazimisha serikali ya Kenya kuzizuia ndege zote kutua, sasa umedhibitiwa, huku uchunguzi ukiendelea.
Waziri wa Usafiri na Miundombinu, Michael Kamau, anaongoza upelelezi huo. Rais Uhuru Kenyatta na mawaziri kadhaa wamekuwapo kwenye uwanja huo wa ndege tangu mapema asubuhi ya leo (Jumatano, 7 Agosti) , mara tu baada ya taarifa za moto kusambaa.
Moshi mzito na cheche za moto zimeonekana mapema asubuhi kwenye anga la uwanja huo wa ndege, zikitokea kwenye sehemu za kuwasili na kusafiri abiria wa ndege za kimataifa.
Hakuna taarifa za watu waliouawa ama kujeruhiwa hadi sasa, na abiria waliokuwa kwenye ndege ambazo zilikuwa tayari zimeshatua wakati moto huo ulipozuka, walifanikiwa kuondolewa salama.
Maafisa wa serikali wanasema sehemu ya paa la Kitengo Namba 1 cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta lilianguka kutokana na moto huo, na kuwapa tabu sana wafanyakazi wa kikosi cha uokozi kupambana na moto huo ulioanza mapema asubuhi.

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)