Dar. Serikali imetangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma itakayoanza kutumika mwezi huu, huku kima cha chini kikiongezwa kwa asilimia 41.18 kutoka Sh 170,000 hadi Sh240,000.
Vilevile, mishahara ya watumishi wengine wa umma imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41. Waraka namba moja kwa watumishi wa umma uliotolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi Julai 2 mwaka huu, unaeleza kuwa marekebisho hayo ya mishahara yatahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa.
Wengine watakaonufaika na marekebisho hayo ni watumishi walioshikizwa kwenye taasisi za umma na watumishi ambao watakuwa kwenye likizo inayoambatana na kuacha kazi, kustaafu kazi au kumaliza mikataba baada ya Julai mosi mwaka huu.
Waraka huo umeonyesha kuwa watumishi wa serikali ambao wanapata mishahara binafsi isiyo ndani ya viwango vya mishahara ya serikali hawatahusika na marekebisho hayo.
Mei 29 mwaka huu, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, aliliambia Bunge, kwamba Serikali imekamilisha majadiliano ya kuongeza kima cha chini cha mshahara katika sekta 12 binafsi, kitakachoanza kutumika rasmi Julai mosi.
Mei mosi mwaka huu akiwa mkoani Mbeya, Rais Jakaya Kikwete, aliahidi unafuu wa maisha kwa wafanyakazi kwa kuangalia uwezekano pia wa kupunguza kodi kwenye mishahara, Lipa Kadiri Unavyopata (PAYE).
Kuhusu kuongeza mishahara, Rais Kikwete aliahidi wafanyakazi wote kwamba Serikali itaendelea kuiongeza kulingana na hali ya uchumi wa nchi. Waraka huo unaonyesha kuwa mishahara mipya kwa watumishi wa serikali kada ya masharti (operational service), ngazi ya mshahara na mshahara mpya kwenye mabano ni;
TGOS A
TGOS A 1. (Sh240,000), TGOS A 2. (Sh245,600), TGOS A 3. (Sh251,200), TGOS A 4. (Sh256,800), TGOS A 5. (Sh262,400), TGOS A 6. (Sh268,000), TGOS A 7.(Sh272,000), TGOS A 8(Sh279,000), TGOS A 9.(Sh284,800), TGOS A 10(Sh290,400), TGOS A 11(Sh296,000), TGOS A 12(Sh301,600), TGOS A 13(Sh 307,200), TGOS A 14(Sh312,800), TGOS A 15(Sh 318,400), TGOS A 16(Sh324,000), TGOS A 17(Sh329,600) na TGOS A 18(Sh335,200).
TGOS B
TGOS B 1. (Sh347,000), TGOS B 2. (Sh356,500) TGOS B 3 . (Sh366,000), TGOS B 4 . (Sh375,500), TGOS B 5. (Sh385,000), TGOS B 6. (Sh394,500), TGOS B 7. (Sh404,000), TGOS B 8. (Sh413,500), TGOS B 9. (Sh423,000), TGOS B 10. (Sh432,500), TGOS B 11 . (Sh442,000) na TGOS B 12. (Sh451,500).
No comments :
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa