Translate in your language

Friday, October 17, 2014

SURUA NI NINI?

   
Surua ni mojawapo ya magonjwa ya kuambukiza ambao una kiwango cha juu cha maambukizi pindi mtu apatapo vimelea vya ugonjwa huu. Pamoja na kuwepo chanjo ya ugonjwa huu bado Surua ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo vingi va watoto walio chini ya umri wa miaka 5 katika baadhi ya maeneo duniani hasa kwa nchi zinazoendelea.

Surua husababishwa na nini?
        Surua huenezwa na aina ya virusi jamii ya paramyxovirus katika mfumo wa njia ya hewa. Kwa sababu hii basi virusi hawa huenezwa kwa njia ya upumuaji.Baada ya kuingia ndani ya mfumo wa hewa virusi hushambulia seli za utando wa nje wa njia ya hewa (respiratory tract epithelium) na kuingia katika mzunguko wa limfu na kufika kwenye tezi za karibu na kusambaa mwilini.

 Muonekano wa Mgonjwa
     Dalili za awali za Surua huanza kuonekana baada ya siku 8 baada ya kupata maambukizi. Mgonjwa huwa na mafua mepesi, homa, kukohoa na macho kuwa makundu. Baada ya siku 2-4 tangu kuanza kuonekana kwa dalili za awali.Ukimchunguza mdomo wa mtoto, ndani ya shavu utaona vidonda vyeupe (koplik spot) kwenye utando mwekundu wa ndani ya mdomo. Hii ni dalili tosha ya kudhibitisha uwepo wa Surua. Lakini vilevile mgonjwa anaweza kuwa na vipele vidogo sana ambavyo huanzia usoni au nyuma ya sikio na kushuka chini kabla ya kutapakaa mwili mzima.

Athari za Surua
    Surua husababisha maambukizi njia ya masikio, mfumo wa hewa (nimonia), ubongo (encephalitis), misuli ya moyo (myocarditis). Surua inaweza kusababisha utapiamulo, upungufu wa  chembe sahani kwenye damu( thrombocytopenia)

Matibabu
   Hakuna tiba maalum kwa ajili ya Surua. Lengo kubwa la matibabu ya Surua ni kuhakikisha mgonjwa anapata mapumziko, maji ya kutosha na dawa ya kutuliza homa kama paracetamol.
 Kinga ya Surua
        Surua huzuiwa kwa urahisi kwa njia ya chanjo. Watoto ambao hawajapata chanjo ya Surua wapo katika hatari kubwa sana ya kupata Surua.




No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)