Shule ya Sekondari Lilasia yafanya mahafali ya 6.
*Wataka kuwe na lugha maalum mashuleni
NA ANDREW CHALE
NJIA nyepesi ya kukabiliana na tatizo kubwa la ajira kwa vijana nchini ni kuongeza kasi ya uwekezaji kwenye viwanda, sanjari na kuutazama upya mtaala wa kufundishia kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu, hususan kwenye eneo la lugha, imeelezwa
Aidha, Lyimo, ambaye kitaaluma ni mwalimu anayehudumu kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 25 sasa, ameshauri yafanyike mabadiliko ya mtaala hususan kwenye lugha ya kufundishia, huku akisisitiza ni wakati mwafaka sasa kwa taifa kuamua ni lugha ipi itumike kufundishia kama ni Kiingereza au Kiswahili, tofauti na ilivyo sasa kuchanganya changanya.
Hata hivyo, katika hatua nyingine, aliwaomba wafadhili kujitokeza kuchangia shule hiyo kwenye eneo la upatikanaji wa maabara ya kisasa, ikizingatiwa shule kwa sasa pamoja na mambo mengine inasomesha watoto yatima bure na kusaidia kwa kiasi utoaji wa elimu bora kwa watoto wa Kitunda na kwingineko nchini
"Tunaomba pia serikali igeuzie macho kwenye shule hii, tuna watoto yatima hapa, itusukume kwenye kupata ruzuku sababu tunasaidia taifa na hata ada tunazopokea ni ndogo mno," alisema
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Lilasia, Silas Kamando alisema katika mahafali hayo jumla ya wanafunzi 36 wakiwemo wanaume 17 na wasichana 19 wamehitimu kidato cha nne mwaka huu, na kwa sasa wanajiandaa na mtihani wao wa taifa unaotarajia kufanyika Novemba 3 mwaka huu, nchini kote
No comments :
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa