Translate in your language

Friday, May 31, 2013

Tunaomba radhi kwa picha hii ya Mangwea

NDUGU wadau tunaomba radhi kwa kuwaletea picha hii ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Albert Mangwea aliyefariki Dunia juzi nchini Afrika Kusini,tunatambua kuwa picha hii si nzuri lakini tumelazimika kuwaletea ili mshuhudie jinsi mpendwa wetu alivyokuwa kabla ya kutengenezwa.
Kiukweli Mangwea alikufa kifo cha masikitiko, msanii huyo aliyewai kutamba na wimbo wa Geto langu pamoja na mikasi iliyotengenezwa na mwaandaaji wa ala za muziki nchini Tanzania P Funk Majani.
Mangwea alikutwa amekufa katika chumba walichokuwa wamelala na msanii wa mwenzake M 2 The P, Mangwea alikutwa amelowa damu nyingi, ambazo zilikuwa zikitoka kwa wingi kupitia mdomo,pua na masikio
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wameiambia Habarimpya.com kwamba kitendo cha msanii huyo kuvuja damu nyingi ndiyo iliyosababisha kifo chake na kwamba hata jopo la Madaktari waliompokea walishangazwa na damu hizo kabla ya uchunguzi kufanyika.
chanzo: Habarimpya.com

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)