Translate in your language

Wednesday, February 24, 2010

MAPUMZIKO YA SIKUKUU YA MAULID KITAIFA

 
Sherehe za Maulid mwaka huu kitaifa zitafanyika mjini Mtwara.
Taarifa zilizopatikana kutoka Ofisi ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania zinasema kuwa, maadhimisho hayo ya Maulid yatafanyika usiku wa Ijumaa tarehe 26 Februari, 2010 kuamkia Jumamosi 27 Februari, 2010. Kufuatia maadhimisho hayo, siku ya tarehe 27 Februari 2010 itakuwa ni siku ya mapumziko kote nchini sawa na mwezi 12 Mfungo Sita. Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) linawatakia mapumziko mema Watanzania wote.
 
chanzo:MICHUZI JR

No comments :

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa

Kijiweni (nipe 5)