Na Mwanablog wetu
UBALOZI wa Marekani Dar es Salaam umeungana na mabalozi mengine duniani kwa kutumia fomu mpya za DS -160 kwa ajiri ya maombi ya matembezi ya muda mfupi itakayoanza kutumika kuanzia Mei 31 mwaka huu.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Ubalozi huo jana jjini
Taarifa hiyo ilielezea kuwa; Idara ya Uhamiaji, Wizara ya mambo ya nje Marekani imeboresha DS-160 kwa wale waombaji wote wa aina hiyoo ya muda mfupi (NIV) Fomu hii italeta mabadiliko kwenye fomu zote zinazopatikana kwenye mtandao (EVAF).
Mabadiliko ya Viza DS-160, yataleta mabadiliko kwenye hatua ya kwanza ya maombi pamoja na faida nyingi kwa waombaji wa viza Dar es Salaam ambao tayari wameisha jaza fomu zao kupitia kwenye mtandao'.alieleza taarifa hiyo.
Katika fomu hiyo mpya, tofauti yake ni kwa waombaji kutuma maombi
Kwa hali hiyo, kila mmoja anahitajika kujibu maswali yote ili kuepusha usumbufu ambao ubalozi itabidi wakurudishe kutokana na kutokamilika kwa fomu zako. Pia watapata kujipangia muda (miadi).
Ikifafanua zaidi taarifa hiyo, ilisema uchunguzi uliofanywa na huduma kwa wateja Duniani kote, umeonyesha mafanikio makubwa ya kuridhisha na fomu hiyoo mpya muombaji wa Viza atatakiwa kuleta uthibitisho wa kupokelewa kwa maombi yake Ubalozini wakati wa mahojiano.
Mitandao na tovuti ambayo fomu hizo za DS -160 inapatikana na kupata maelezo ya hatua kwa hatua ni kupitia ; http://www.tanzania.usembassy.gov ama kutembelea katika ofisi za balozi hizo ama kuwasiliana na idara ya uhamiaji kwa barua pepe drsniv@state.gov.
Mwisho
No comments:
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa