PICHANI
Askari polisi wa kituo cha Iringa wakituliza fujo kati ya wachezaji wa timu ya Kinondoni na Mapinduzi stars kutoka Mbeya baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa mwisho wa Kili taifa Cup uliokuwa ukichezwa katika uwanja wa Samora jana na timu hizo kutoka bila kufungana huku Iringa ikiwa bingwa wa kituo hicho kwa kuifunga Rukwa kwa goli 6-0.
Mashindoni ya Kili Taifa Cup kituo cha Iringa yamelazika kwa mapigano makali kati ya wachezaji wa timu ya Mapinduzi Stars kutoka mkoa wa Mbeya na Kinondoni baada ya timu hizo kutoka sare na kutuhumiana kupokea rushwa kutoka kwa wenyeji Iringa. Mapigano hayo ambayo yalipelekea polisi kuingilia kati huku baadhi ya askari polisi wakitumia mikanda ya suruali zao zao kutumia kama silaha za kuwasambaza mashabiki na wachezaji hao ambao walikuwa katika vita kali ya kurushiana mawe huku wanahabari wakipokea kipigo kutoka kwa wachezaji wa Kinondoni ambao walionekana kugeuka mbogo baada ya kupoteza ubingwa katika kituo hicho . Mwandishi wa habari hizi ambaye alikuwa ni mmoja kati wa wanahabari waliopokea kichapo kutoka kwa wachezaji wa Kinondoni ambao walikuwa wakiwaadhibu wahasimu wao Mbeya kwa madai ya kuuza kupokea rushwa kutoka kwa Iringa ili kukaza katika mchezo kati yake ya Kinondoni. Katika vurugu hizo zilizodumu kwa zaidi ya dakika 20 baada ya mchezo huo kumalizika polisi zaidi ya 10 ndio ambao walikuwepo uwanjani hapo huku wakiwa mikono mitupu bila kirungu wala silaha yoyote ya kutuliza ghasia ,waliweza kupata wakati mugumu kutuliza vurugu hizo ambapo baadhi yao walipata kipigo kutoka kwa mashabi hao ambao walikuwa wakirusha mawe. Baadhi ya mashabiki wa soka wa timu ya mkoa wa Iringa wakiongozwa na Shukuru Lwambati walilazimika kujitumbukiza katika vurugu hizo ili kuwasaidia kuwaokoa wachezaji wa Mbeya ambao walikuwa wamezidiwa nguvu na vijana hao wa Kinondoni katika vurugu hizo. Wakizungumza baada ya mchezo huo mashabiki wa soka wa timu ya mkoa wa Iringa mbali ya kuipongeza timu yao kupita kwa kishindo cha magoli 6-0 dhidi ya Pinda Boys (Rukwa ) katika mchezo wake wa mwisho na kuifanya timu hiyo ya mkoa wa Iringa kuwa timu pekee katika kituo hicho kwa kuwa na pointi nyingi na magoli 9 na pointi 10 ikifuatiwa na Kinondoni yenye magoli 5. Mashabiki hao walisema kuwa sababu ya kinondoni kufanya fujo ni kutokana na kujiwekea malengo makubwa ya kushindwa katika kituo hicho jambo ambalo limeonekana kwenda ndivyo sivyo baada ya wenyeji Iringa kushinda na kuwa bila viongozi wa Kinondoni kuhamasisha wachezaji wao kufanya fujo katika uwanja huo wa Samora damu zisingemwagika . Hata hivyo katibu wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa (IRFA) Eliud Mvella alipofuatwa na mwandishi wa habari hizi ili kuzungumzia fujo hizo aligoma kuzungumza na kuishia kutamka maneno mawili pekee ambayo ni No Coment. Hizi ni fujo za pili kufanywa na Kinondoni toka kuanze kwa mashinadno hayo ambapo fujo zinazolingana na hizo walizifanya wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo baada ya kutoka sare ya goli 1-1 na Iringa na hivyo kufanya fujo mbele ya mkuu wa mkoa wa Iringa Mohamed Abdulaziz pamoja na katibu mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela
|
|
No comments:
Post a Comment
here u,re comments/acha ujumbe wako hapa