Friday, April 16, 2010

   UPIGAJI 'KIPUSA' MARUFUKU SHULENI SOMALIA
 
Waalimu katika mji mmoja nchini Somalia wamesema
wanaharakati wa Kiislamu wameamrisha
shule kuacha mara moja kutumia kengele kutenganisha
kipindi kimoja na kingine wakati wa
masomo shuleni.
Wapiganaji hao wamesema milio ya kengele hizo ni sawa
na ile inayosikika makanisani.
Mwalimu mmoja ameambia BBC kundi la Al Shabaab
limesema waalimu wa shule zitakazokaidi
amri hiyo watapelekwa mbele ya mahakama za Kiislamu
ama Sharia.
Mwalimu mkuu kutoka shule moja amesema kundi la
Al Shabaab pia limeamrisha historia ya vita
vya Jihad kuwekwa kwenye mitaala. Tayari kundi hilo limepiga
marufuku muziki kupigwa katika
maeneo inayodhibitili na pia redioni.

No comments:

Post a Comment

here u,re comments/acha ujumbe wako hapa